HABARI BINAFSI
Kwa majina ni: LUKA ROKI CHAMAYOMBE.
Jina hili la tatu siyo jina la ukoo; wala si jina la babu yangu bali
ni jina ambalo baba yangu alijipa mwenyewe na mimi naliendeleza tu. Jina
la babu ni “SESIYAMOTO” maana “CHECHEYAMOTO” Majina yangu ya uzaliwa/ukoo ni Kusinile, Maghali au Mihengo.
Nimezaliwa
tarehe 8/4/1937 katika kitongoji cha Misegese, Tarafa ya Mlali, Wilaya
ya Morogoro Vijijini, wakati huo (kwa sasa Wilaya ya Mvomero) Mkoani
Morogoro. Nimebatizwa tarehe 26/5/1937 Parokia ya Mgeta, Jimbo la
Morogoro.
Kimasomo,
kwa muda wa miaka kadhaa hadi 1949 nilisoma Bush School ya Peko. Miaka
1950-1952 niliendelea na elimu ya msingi hadi darasa la IV katika shule
ya msingi Kigurunyembe. Miaka 1953-1959 niliendelea na masomo Bagamoyo
Seminari ndogo ya Mt. Petro. Miaka 1960-1961 niliendelea na masomso
katika Seminari ndogo ya Mt. Maria Nyegezi Mwanza, ambako nilifannyia na
kufuzu mitihani ya “Cambridge” ya Darasa la XII. Miaka 1961-1962
nikaendelea na masomo katika Seminari Kubwa ya Mt. Thomas Kilakala
Morogoro. Kutokana na kufungwa kwa Seminari Kubwa ya Mt. Thomas mwaka
1963 nikahamia Seminari Kubwa ya Kipalapala Mkoani Tabora ambako
mwishoni mwa mwaka 1966 nikafanikiwa kuacha kusomea upadre kwa kukubali
kwenda kufundisha Seminari Ndogo ya Mt. Pius Makoko Wilayani Musoma mkoa
wa Mara kwa Mwaka mmoja 1967.
Mwaka
1968 nikaajiriwa Serikalini katika Wizara ya Maendeleo Vijijini. Miaka
1976-1979 nilipata likizo ya miaka 3 ambayo nilitumia kusomea “Advanced
Diploma in Business Administration” IDM Mzumbe Morogoro. Baada ya Masomo
hayo nikahamishiwa Wizara ya Biashara hadi nilipostaafu kama Afisa
Biashara Mwandamizi III mnamo April 1992.
Mwaka
1995 nikajiunga na Karismatiki Katoliki Mzumbe, Morogoro. Tangu hapo
nikawa miongoni mwa wapeleka Injili Maparokiani Jimboni Morogoro; na nje
ya Jimbo la Morogoro kama vile Iringa, Ilongero-Singida,
Kigonsela-Mbinga, Ngaramtoni mkoani Arusha na Ngong’ nchini Kenya.
Lakini
kadiri nilivyoukulia ukweli wa Mungu ndivyo wengi walivyoshindwa
kunielewa kabisa. Hata ikafikia wakati nikanyimwa fursa ya kuhubiri. Kwa
ufahamu niliokuwa nimeufikia katika kuukulia ukweli wa Mungu,
nikayapuuza hayo yote. Nikaamua kusonga mbele na wale tu wasiopenda
utukufu wa mwanadamu kuliko utukufu wa Mungu (Yn.5:41,44; 12:43). Nami,
katika uwanja wa kuukulia ukweli wa Mungu, nikawa namuhesabu mtu yeyote
anayependa utukufu wa wanadamu kuliko wa Mungu kweli, kuwa ni fira.
Hivyo, hiyo imekuwa ndiyo hali halisi katika kuukulia ukweli wa Mungu wa
pekee wa kweli.
Mungu
hutaka watu wote waokolewe na kupata kujua iliyo kweli (1Tim.2:4),
maana watu wake hupotea kwa sababu ya kutojua maandiko wala uweza wa
Mungu (Mt 22:29). Hatimaye atuambia, “mkiyajua hayo, heri ninyi
mkiyatenda”. (Yn 13:17) na kinyume cha “Heri” ni “Ole”. Hivyo, kwa
sababu zilizotolewa katika Ebr.6:4-6 na 2 Pet.2:20-22, mimi sitarudi
nyuma. Kwa utendaji wa Mungu Roho aliye katika Nafsi Tatu: Kweli, Neno
na Roho wa kweli, hakuna neno lolote lisilowezekana; bali kuna kushinda
na zaidi ya kushinda kwa Yeye atupendaye upeo (Yn.13:1) kwa upendo wa
milele (Yer.31:3) na ambaye haachi kujishughulisha kwa mambo yetu
(1Pet. 5:7); maaana Yeye aweza kufanya mambo ya ajabu mno, kuliko yote
tuombayo au tuwazayo kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu milele
yote (Efe.3:20).
Kwa
utendaji wa Roho Mtakatifu nafsini mwangu, ninaamini kikwelikweli 100%
kwamba nahesabiwa kuwa mwenye haki wa Mungu kutokana na neema au zawadi
ya Damu ya Yesu Kristo Neno la Mungu. Naamini kwamba utakaso huo
umefuatiwa mara moja na kunyweshwa Roho Mtakatifu na kumvaa Kristo Neno
la Mungu kuwa Roho moja Naye; Kristo yu ndani yangu nami nimo ndani
yake. Na hivyo, Mungu Roho aliye katika Nafsi Tatu yumo ndani yangu,
nami ndani yake. Hivyo, ufalme wa mbinguni umo ndani yangu kwa sababu
Mungu Roho aliye Nafsi Tatu Yumo ndani yangu hapa duniani, nami nimo
ndani yake katika ulimwengu wake wa Roho, Mbinguni. Haniachi yatima.
Yuko nami kotekote wakati wote. Hivyo niko mzima, salama na mshindi
katika yote wakati wote. Ni raia ya ufalme wa Mungu pekee wa kweli
(Phil. 3:20), kwa huyo Roho wa kweli niliyenyweshwa (1Kori 12:13: 1Yoh
3:24).



0 comments:
Post a Comment