Subscribe:

Sample text

Sample Text

Wednesday, 4 October 2017

BIKIRA MARIA MAMA WA MKOMBOZI NA MAMA YETU MZAZI

Miongoni mwa maswala nyeti ambayo Papa Yohani Paulo II aliagiza yajifunzwe kwa upya ni swala la Mama yetu Bikira Maria (The Call for Christian Unity (Kifungu cha 79).
Katika uhalisia wa mambo ni kwamba ubinadamu unakabiliwa na tatizo la utumwa wa dhambi unaotokana na dhambi ambayo imepelekea ulimwengu huu kuwa chini ya miliki ya Yule mwovu.
MPANGO WA UKOMBOZI
Mshahara wa dhambi ni mauti (Rumi 6:23). Watu wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu (Rumi 3:23). Hivyo, kiuhalisia watu wote wamekufa, ni maiti.
Ili kurejesha uzima, ilibidi Yeye mwenyewe arudi ndani ya mtu wake aliyejifarakanisha kwa kumwamini Yule mwovu. Na haiwezekani arudi ndani ya mtu wake hali dhambi ingalimo ndani yake.
Katika hali yake ya umauti, na kutokana na hali ya dhambi kuwa ukuta au kiambaza kati yake Mungu na mtu wake, mtu hawezi kufanya lolote lile kujikwamua kutoka utumwa wa dhambi.
Ndipo Yeye mwenyewe akamua kushiriki ubinadamu, ili Yeye mwenyewe katika hali ya kibinadamu amharibu shetani (Ebr.2:11-17), kuifuta na kuiondoa dhambi isiwepo tena; na hivyo kufuta enzi na mamlaka ya shetani (Kol.2:13-15).
Kukamilisha kusudio hili la kushiriki hali ya kibinadamu, akamteua Bikira Maria, ambaye amekubali na kubarikiwa kwa utakaso na kuingiwa na Roho Mtakatifu. Na kadiri ya 1Yoh.4:13, kwa huko kushirikishwa Roho Mtakatifu, Bikira Maria akawa ndani ya Mungu na Mungu ndani ya Bikira Maria, akawa umoja na Mungu katika Utatu wake Mtakatifu, tayari kutimiza kazi ya ukombozi kama ilivyokusudiwa.
Hivyo katika kutimiza kazi ya ukombozi Bikira Maria hayuko nje ya Mungu katika Utatu wake Mtakatifu.
BIKIRA MARIA MAMA MZAZI WA WAZALIWA MARA YA PILI
Bikira Maria ni Mama wa Yesu ambaye ni Neno la Mungu aliyefanyika Mwili (Yn.1:14).Tumboni mwa Bikira Maria.
Wale ambao kiuhalisia wanaambiwa “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili kwa mbegu isiyoharibika, kwa Neno la Mungu lenye uzima lidumulo hata milele (1Pet.1:23); hao ndio wale wanaosemekana katika Ebr.2:11, “Maana Yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja; kwa ajili hii Yesu haoni haya kuwaita ndugu zake.
Atakasaye ni Neno aliyefanyika Mwili. Wanaotakaswa ni hao waliozaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu lidumulo hata milele. Wote wamezaliwa na Neno la Mungu. Neno la Mungu ndiyo mbegu ya kiume iliyowazaa. Ni ndugu, ni makaka “Brothers)” siyo “Half-Brothers”).
Maadamu sisi nasi tumezaliwa kwa Neno la Mungu, Yesu Neno la Mungu aliyefanyika Mwili tumboni mwa Bikira Maria, sisi tuliyezaliwa kwa Neno la Mungu nasi tulikuwa naye tumboni mwa Bikira Maria. Alipomzaa Yesu katuzaa pamoja na Yesu.
Hivyo, kiuhalisia, Bikira Maria ni Mama yetu mzazi wala si mama wa Kambo.
BIKIRA MARIA WA MLIMA KARMERI NA BIKIRA MARIA WA FATIMA
Je, Bikira Maria anayehusika na matumizi ya Skapulari iliyoandikwa, “Whoever dies wearing this Scapular will never suffer eternal hell” na Bikira Maria wa Fatima aliyetuhimiza kusali rosari, ni Bikira Maria wa kweli?
Tumeagizwa kuzipima roho, maana kuna Roho wa kweli na roho ya upotevu (1Yoh.4:1, 6). Bikira Maria wa kweli kamzaa Yesu wa kuwaokoa watu wake kutoka utumwa wa dhambi (Mt.1:21). Sasa Bikira Maria anayehimiza taratibu ambazo hazisaidii kitu kuokoa watu kutoka utumwa wa dhambi, huyo anaweza kuwa Bikira Maria wa kweli? Je, huyo atakuwa nje ya Yule mwasi ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho mungu au cha kuabudiwa? Yule ambaye huketi hata katika hekalu la Mungu, akijionesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu? (2thes.2:4)
Kwenye Mabanda ya Huduma ya Kufunguliwa, wanapelekwa watu wenye mapepo ambao wamevaa rosari na Skapulari. Kama vitu hivi vina nguvu ya Mungu pekee wa kweli, mapepo yanaishije na watu waliovaa vitu hivi? Na kama yanaweza kuishi nao wanovaa vitu hivi, yatashindwaje kuwasindikiza kuzimu mwishoni mwa maisha yao hapa duniani?
Ikiwa ibada wanazoenenda nazo (kuungama, kuhudhuria Misa, kukomunika, kutoa zaka na sadaka) hazifai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili (Kol.2:23; Gal.5:19-21), yaani, hazifai kitu kulikabili tatizo la utumwa wa dhambi. Ibada hizo anapofanyiwa akiisha kufa zitapata wapi nguvu ya kuweza kutatua tatizo la dhambi?
Hivi, ibada hizi haziishii kuwa mchezo wa kuigiza tu? Nakubaliana na agizo la Papa Yohani Paulo II kwamba tuwe waaminifu kwa Injili tuwe na fikira mpya, mtazamo mpya wa mambo na wongofu wa kina.
Kwa usalama wetu tuzingatie agizo hili ambalo linatokana na Mtaguso wa Vatikani II. Mungu anataka watu wote waokolewe na kupata kujua iliyo kweli (1Tim 2:4). Maana watu wake wanapotea kwa kuwa hawajui Maandiko wala uwezo wa Mungu (Mt.22:29). Na njia ya kujua kweli ni kukaa katika Neno lake; ndipo tutakapo kuwa wanafunzi wake Yesu kiukweli, na kujua kweli itakayotuweka huru (Yn.8:31-32).
Ibada hizo kwa Bikira Mria ni ibada zilizo laaniwa kwa sababu
• Ziki nje kabisa ya injili iliyohubiriwa na mitume wa Kristo Neno la MUNGU.
• Zinawapambanisha Kristo Neno la Mungu mbaye, kwa kadiri ya mapango wa MUNGU, ndiye Mwombezi( Rum.8:26-27,34; ebr.2:17; 7:25; 1Yoh.2:1-2).
• Kadiri ya 1Yoh.4:13, Bikira Maria ni mshiriki wa umoja wa nafsi tatu za MUNGU. Hivyo ,fikra za kumchomoa Bikira Maria awe nje ya utatu mtakatifu wa Mungu ni fikra farakanishi amabazo ni za yule mwovu. Hatupaswi kuafikiana naye.
Ni ujumbe kutoka kwa nduguyo katika Neno la Mungu, la Mungu aliyefanyika Mwili kututoa kwenye utumwa wa dhambi. Tumshukuru kwa Roho Mtakatifu.
LUKA ROKI MAGHALI CHAMAYOMBE
0714 118 428
0787 765 759
0753 298 707
Email: chamayombe37@gmail.com

0 comments:

Post a Comment