1. Kanisa la Yesu ni moja Takatifu, Katoliki na la kimitume. Kwamba
Kanisa la Yesu ni moja ni kwa sababu, kwa njia ya Kristo, pamoja naye
na ndani yake, kila mdau wa Kanisa la Yesu yuko ndani ya kila Nafsi ya
umoja wa Nafsi Tatu za Mungu; na kila Nafsi ya Utatu Mtakatifu yuko
ndani ya kila mdau wa Kanisa la Yesu. Na kwa utaratibu huo ni kwamba
kila mdau wa Kanisa la Yesu yuko ndani ya kila mdau wa Kanisa la Yesu
(Yn.17:21-23). Kwa jinsi hii wadau wa Kanisa la Yesu, kwa pamoja huwa
maskani moja ya Mungu pekee wa kweli katika Roho (Efe.2:18-22)
2.
Kanisa la Yesu ni Takatifu kwa sababu hutakaswa sawasawa na maombezi ya
Yesu (Yn.17:17, 19), na kwa Neno la Mungu kweli (Efe.5:25-27);
Ebr.10:1923). Na kwa utakaso huo hukamilishwa katika Umungu huo kwa
kunyweshwa Roho wa kweli (1Kor.12:13). Na hivyo kumvaa Kristo kushiriki
utimilifu wa Mungu. Katika hali hiyo, hatendi tena dhambi (Yoh.3:6, 9;
5:18).
3. Kanisa la Yesu ni Katoliki. Neno Katoliki” maana yake halina mipaka (Universal).
Sasa Kanisa la Yesu ni Katoliki kwa sababu kwanza Yesu alionja mauti
kwa ajili ya kila mtu (Ebr.2:9); ili kujikusanyia watu wake
waliotawanyika wawe wamoja tena (Yn.11:52), chini ya Mchungaji Mmoja
(Yn.10:16); kuwanywesha Roho mmoja ili wawe mwili mmoja (1Kor.12:13); na
hivyo kumvaa Yesu bila ubaguzi wowote (Gal.3:27). Ili kuwa Roho moja
na Yesu (1Kor.6:17) na hivyo kuwa mdau wa Kanisa na Yesu (Gal.3:29;
Rum.8:9) popote pale walipo.
4. KANISA LA YESU ni LA KIMITUME
Kwa kadiri ya Yn..11:52, Kanisa la Yesu ni kusanyiko la watoto wa Mungu
waliotawanyika ili wawe wamoja tena. Mitume walikuwa wa kwanza
kuchaguliwa wawe Kanisa moja la Yesu. Kwa muda wa miaka mitatu
wakaandaliwa jinsi ya kuwa wadau wa Kanisa la Yesu.
Ili kuwa mdau
wa Kanisa la Yesu sharti mtu awe Roho moja na Yesu (1Kor.6:17) kwa
kunyweshwa Roho wa kweli (1Kor.1Kor.12:23) ili hivi kwamba mtu kuwa
ndani ya Mungu na Mungu ndani ya mtu, kuwa umoja na Mungu (1Yn.4:13).
Hivyo ndivyo mtu huwa wa Yesu kweli (Gal.3:29; Rumi 8:9).
Katika
hali hiyo mtu amekuwa amezaliwa mara ya pili katika Umungu pekee wa
kweli (Yn.3:3, 5; Gal.3:26). Ili hili lipate kutendeka, sharti mtu
apokee, ile neema au zawadi ya upatanisho kwa njia ya imani katika Damu
ya Yesu; (Rumi 3:24—26; Ebr.10:19-23). Kwani haitawezekana Mungu kurudi
ndani ya mtu kabla ya Upatanisho.
Kwa kupokea upatanisho kwa
njia ya imani katika Damu ya Yesu, Mungu Baba huziachilia katika
ustahimili wake dhambi zote zilizotangulia kufanywa (Rum.3:25); na
kumhesabia mtu husika haki katika Kristo Yesu (2Kor.5:21).
Pamoja
na Yesu kuwafundisha mitume wake mengi kuhusu Ufalme wa mbinguni,
lakini katika Yn.16:12-15. Bwana Yesu awaambia mitume wake “Hata bado
ningali ninayo mengi ya kuwaambia lakini, hamwezi kuyastahimili hivi
sasa. Lakini Yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie
kwenye kweli yote ….”. Kujua mambo ya Mungu, sharti mtu awe na Roho wa
Mungu. Na Roho wa Mungu hupatikana baada ya Yesu kutukuzwa (Yn.7:39)
Hii inatukumbusha kile Yesu alichokisema kuhusu mito ya maji yaliyo hai
ambayo hutoka ndani yake yeye aaminiye. Wakati huo Roho huyo alikuwa
hajaja kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa (Yn.7:37-39).
Hii
inamaanisha kwamba lile swala kuu la jinsi ya ujio wa Roho wa kweli na
jinsi ya uendeshaji wa Kanisa lake na mengineyo mengi, Yesu hakuwaambia
Mitume wake kwa sababu ni maswala yanayotendwa na Roho wa kweli mwenyewe
akiwa ndani yake mtu husika; kama anavyo-tuambia katika 1Kor.2:12,
“Lakini sisi hatukupokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu,
makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu: (Soma 1Kor.2:10-16).
Mitume walimpokea Roho wa kweli pale walipovuviwa na Yesu na kuambiwa
pokeeni Roho Mtakatifu (Yn.20:22). Tangu hapo Bwana Yesu kwa huyo Roho
wake wa kweli akakamilisha ngwe nzito iliyobaki ambayo sisi sasa
twaipata katika nyaraka zao hawa mitume, huyo Roho wa kweli na jinsi ya
kumpata.
Kwa sababu hiyo, kupuuza Nyaraka za Mitume ni janga
kubwa mno ambalo mtu huweza kujiingiza kwa hasara yake mwenyewe na hata
wale anaowaongoza, ikiwa mtu huyo ni Kiongozi. Kweli yote kuhusu elimu
ya ufalme wa mbinguni hupatikana katika Nyaraka za Mitume. Kuhubiri
habari za Yesu nje ya mahubiri ya Mitume ni laana (Gal.1:8-9) kwa sababu
hayo yatakuwa ni mahubiri yalio nje ya kweli yote. Yn.16:12-13)
aliyotuletea Bwana Yesu.
Kwa kufanya dhambi ya kuwapuuza Mitume
wa Yesu, badala ya kuhubiri taratibu za kuondokana na utumwa wa dhambi,
Makanisa huishia kuhubiri mungu pesa kwa masilahi ya wahusika. Badala ya
kumhubiri Mungu wa Mbinguni, makanisa humhubiri mungu wa kuzimu kwa
maangamizi ya wahubiri na wahubiriwa, wenyewe bila kujua. Ni HATARI!
5. KANISA LA YESU NI LA ULIMWENGU WA MBINGUNI
Pamoja na sifa nne hapo juu, kutokana na ile simulizi ya Tajiri na
Lazaro (Lk.16:19-31), na kujifunua kwa Bwana Yesu, Neno la Mungu, kwamba
Yesu ni wa juu, si wa Ulimwengu huu (Yn.8:23) tunajifunza kwamba mtu
hukabiliwa na aina mbili za ulimwengu; yaani ulimwengu wa Mungu wa
mbinguni na ulimwengu wa kuzimu, kule yule mwasi alikoshushwa kutokana
na dhambi yake ya kujikweza (Isa 14:13-15).
Katika kutuombea kwa
Baba, Bwana Yesu alimwambia Baba “Neno lako nimewapa na ulimwengu
umewachukia kwa sababu wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa
ulimwengu. Mimi siombi kwamba uwatoe ulimwenguni; bali uwalinde na Yule
mwovu; maana wao si wa ulimwengu kama mimi nivyo wa ulimwengu
(Yn.17:14-16). Tena asema, Baba hao ulionipa nataka wawe pamoja nami
popote nilipo (Yn.17:24).
Tena tunasoma, Akatufufua pamoja naye,
akatukatisha pamoja naye katika ulimwengu wa Roho katika Kristo Yesu
(Efe.2:6). Ni akina nani hao? Hao ndio Kanisa la Yesu aliojitakasia
kwa maji katika neno; apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na dosari
wala kunyanzi, wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa
(Efe.5:25-27).
Kwa njia ya Yesu Kristo, wadau wa Kanisa la Yesu
hupata njia ya kumkaribia Baba katika kunyweshwa Roho mmoja(Efe.2:18;
1Kor.12:13). Na katika Kristo Yesu wadau wa Kanisa lake wamejengwa
pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho (Efe.2:22).
Kwa mantiki
hii wadau wa Kanisa la Yesu wanapaswa kwenda kwa Roho (Gal.5:16-17).
Kwa kadiri ya Kol.3:1-3) wanapaswa kutafuta yaliyo juu Kristo aliko;
Kwani Uhai wao umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu (Kol.3:1-3).
Uenyeji wao uko mbinguni (Fil.3:20). Katika umoja wa nafsi Tatu, kweli
na Neno na Roho wa Kweli (1 Yon.5:7 au 8). Wao ni washirika wa tabia ya
Mungu wa mbinguni (2 Pet.1:3-4). Hapa duniani wadau wa Kanisala Yesu
wao ni wageni (1Pet.1:17). Hawapaswi kuipenda dunia (1Yoh.2:15-17).
Nao hutambulikana kwa tunda la Roho (Gal.5:22-23).
Kwa kuwa
Kanisa la Yesu liko katika ulimwengu wa Mungu aliye Roho, Kanisa hili
liko nje ya ile milango 5 ya fahamu za mwili wa nyama; macho, masikio,
pua, ulimi na ngozi. Kanisa la Yesu huenda katika Roho na Kweli kwa
njia ya imani; kwa maana halisi ya neno hili IMANI, yaani kuwa na hakika
ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana (Eb.11:1).
Kama tulivyoagizwa katika Gal.5:16-17 kwenda kwa Roho sifa hii ya
Kanisa la Yesu inahusu pia zile sifa nne za kwanza za Kanisa la Yesu,
kwamba Kanisa la Yesu ni moja Takatifu, Katoliki na la kimitume. Sifa
zote zinapata hadhi katika Mungu pekee wa Kweli ambaye ni Umoja wa Nafsi
Tatu, Kweli na Neno na Roho wa Kweli (1Yoh.507) 8).
Mungu aliye
Roho (Yn.4:24), mwenye Nafsi Tatu, Kweli na Neno na Roho wa Kweli,
amejiumbia mtu wake kwa mfano na sura yake mwenyewe (Mw.1:26) na
kumshirikisha uzima = Roho wake (Mw.2:7) ili kukidhi mapenzi yake ya
kuabudiwa katika Roho na Kweli (Yn.4:23).
Na hilo ndilo Kanisa
lake la Ulimwengu wa Mbingun, ambalo ingawa lipo katika ulimwengu huu,
lakini halienendi kwa kuangalia vinavyoonekana (2Kor.4:18). Ni Kanisa
linaokwenda kwa imani, si kwa kuona (2Kor.5:7). Na Mungu mwenyewe
anasema, “Mwenye haki wangu ataishi kwa imani, naye akisitasita, Roho
yangu haina furaha naye (Ebr.10:28). Kanisa la Yesu ni la ulimwengu wa
mbinguni, ulimwengu wa ROHO.
6. HITIMISHO
Basi kutokana na
hayo, mimi binafsi naamini kwamba ule Waraka wa Kichungaji wa Papa
Yohani Paulo II, “The Call for Christian Unity (ut unum sint) chini ya
uongozi wa Vatikani II, ni uamsho wa kutuamsha sisi sote tuamke na
kuondokana kabisa na huu usingizi wa mauti ya milele unaotukabili.
Waraka hututaka kuwa waaminifu kwa Injili. Pamoja na mengineyo mengi
tunayoagizwa na Injili, Injili hututaka kwenda kwa Roho wala
hatutazitimiza tamaa za mwili ambazo zimeorodheshwa katika Gal.5:19-21,
na ambazo wazitendao hawataurithi ufalme wa Mungu.
Kwamba dhambi
au maasi hushamiri duniani, kama ilivyoshuhudiwa kwenye Kongamano la
Miaka 35 ya Karismatiki Katoliki kule Dodoma, ni kidhibiti tosha kwamba
dunia na dini zake huendeshwa kimwili badala ya kwenda kwa Roho kama
tulivyoagizwa na Injili. Dunia na dini zake zinaiasi Injili.
Tena, kwa mujibu wa mada ya kuzipima roho; ni dhahiri kwamba Roho wa
Kweli amepotezwa. Dunia na dini zake huenenda na roho ya upotevu
inayowafanya watu wa Mungu wampoteze Mungu wao wa kweli. Huenenda na
Roho ya upotevu inayowafanya watu wa Mungu wampoteze Yesu, Neno la Mungu
kweli, na kuenenda na mayesu wengine wa kuzimu.
Sasa wakati
umefika wa kudhamiria kwa dhati ya 100% kwenda kwa Roho kama
tulivyoagizwa na Injili ya Mitume (Gal.5:16-17; 1:8-9).
Wakati wa
kutimilika kwa mapenzi ya Mungu (1Tim.2:4) kwamba watu wote waokolewe
(Kol.1:13) na kupata kujua yaliyo kweli (Yn.17:3) sasa umefika.
Wakati umefika sasa wa kuachana kabisa na fikira za kidini ambazo
huwapelekesha watu wa Mungu kwa makristo wa uongo (Mk.13:21-22); fikira
za kidini ambazo huwapelekesha watu wa Mungu waenende na mayesu wengine
au roho nyingine ambazo huwapelekesha watu wa Mungu mbali kabisa na
Yesu, Neno la Mungu Kweli (2Kor.11:4; Yn.8:26; 3:33).
Wakati
umefika sasa wa kumwambia Yule mungu wa ulimwengu wa kimwili ambaye ni
mwuaji, mwongo na baba wa uongo, wakati umefika sisi dunia tumwambie kwa
ujasiri 100% maadamu tuna Roho wa Kweli, tumwambie, Umetuonea kwa
kutugharagaza katika maasi na maovu yako kiasi cha kutosha. Sasa
tunasema BASI!!!” Tumwambie kwa ujasiri yeye na wafuasi wake, wakome na
wabaki peke yao huko kuzimu, pande za mwisho za shimo walikoshushwa
(Isa.141:15).
Wakati uliokubalika ndio sasa; na siku ya wokovu
ambayo Mungu Kweli huwatakia watu wake ndio sasa; na ndio sasa ambapo
ataka watu wake kujua Kweli.
Ndugu yangu nikupendaye kwa upendo
wa Kristo, fahamu kwamba Nuru ya Yesu imeng’aa gizani wala giza
haikuweza (Yn.1:5). Jipe moyo, Yesu ametushindia (Yn.16:33). Na
ubarikiwe kwa Baraka zote za kiroho katika Ulimwengu wa Roho ndani yake
Kristo, Neno la Mungu Kweli (Efe.1:3), sasa hata na milele!!.....
LUKA ROKI MAGHALI CHAMAYOMBE
0714 118 428
0787 765 759
0753 298 707
Email: chamayombe37@gmail.com
Wednesday, 4 October 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



0 comments:
Post a Comment