Subscribe:

Sample text

Sample Text

Friday, 21 June 2019

KUKULIA UKWELI WA MUNGU: KUKULIA UKWELI WA MUNGU: NI LIPI KANISA LA KRISTO ...





JE,
MBINGUNI YA MUNGU PEKEE WA KWELI IKO WAPI?
Tumehakikishwa
kwamba Mungu pekee wa kweli ni Umoja wa Nafsi Tatu: (1) Kweli (Yn.3:33; 8:26;
1Yoh.1:1-3), (2) Neno (Yn.1:1-5; 1Yoh.1:1-3) na (3) uzima au Roho (Yn.6:63).

1Yoh.5:8
hututhibitishia kwamba Nafsi Tatu hawa hukaa mbinguni katika hali ya umoja
usiogawanyika.






Kwa
mantiki hii tuna kila haki ya kuamini kwamba (1) Nafsi Kweli hukaa katika Nafsi
Neno na Nafsi Uzima au Roho; (2) Nafsi Roho au Uzima hukaa katika Nafsi Kweli,
na Nafsi Neno; na (3) Nafsi Neno naye hukaa katika Nafsi Kweli na Nafsi Uzima
au Roho.


Kifupi
ni kwamba kila Nafsi miongoni mwao hukaa katika kila Nafsi miongoni mwao.


Hivyo,
wanaoshuhudia mbinguni iliyo maskani au kao la Nafsi hao watatu ni Umoja wa hao
Nafsi Tatu miongoni mwao. Umoja wa Nafsi Tatu ndio mbinguni halisi anakokaa
Mungu Umoja wa Nafsi Tatu: Kweli, Neno na Uzima (1Yoh.5:8).

Hivyo
Nyumba ya Mungu tunayoikuta Ebr.10:21, Efe.2:19, Hekalu na Maskani tunayokuta
katika Efe.2:21 na 22 na Patakatifu tupatapo katika Ebr.10:19 si chochote kile
bali Umoja wa Nafsi Tatu za Mungu pekee wa Kweli na ndiyo mbinguni wanakokaa
Nafsi Tatu za Mungu pekee wa kweli.


Tamani
kuingia mbinguni leo kwa njia ya Kristo Neno la Mungu aliye katika Utatu
Mtakatifu, na aliyetuombea kwamba pale alipo na sisi tuwepo (Yn.17:24). Yeye
ndiye aliye Njia, Kweli na Uzima (Yn.14:6) na ndiye Mwombezi wetu (Yn.17; Rum 8:34;
Ebr. 7:25; 1Yoh.2:1). Hakuna Mwombezi wa uhakika na aliyelipa fidia ya
kukubalika kwa Baba ila Yeye tu.

Hatuna
cha kufanya ila kumshukuru Mungu kwa wema, huruma, ukarimu, uwezo na upendo
wake bila mipaka yoyote katika yote. (Efe.3:20).
LUKA
ROKI CHAMAYOMBE
0714118428

0 comments:

Post a Comment