Subscribe:

Sample text

Sample Text

Wednesday, 4 October 2017

WAKARISMATIKI WAKATOLIKI KUWA WAKARISMATIKI KWELI KWELI NA WAKATOLIKI KWELI KWELI

Kati ya vipengere hivi viwili, “Karismatiki”na “Katoliki”, kipengere “Katoliki” kimekwisha kushughulikiwa katika mada iliyoitwa “KANISA LA KRISTO NENO LA MUNGU”. Hivyo, hapa tutajikita katika kujifunza kipengere “KARISMATIKI”.
Katika mada iliyohusu IMANI tumepitia fundisho la Mitume wa Kristo Neno la Mungu kuhusu ukombozi, upatanisho, ondoleo la dhambi au utakaso kwa njia ya IMANI katika Damu ya Kristo Yesu.
Lakini utakaso si jambo linaloishia hewani. Utakaso ni kuondoa kizingiti au kifarakanishi. Kifarakanishi kinaondolewa ili iweje?
Ebr.10:14 hutuambia, “Lakini kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa, Kumbe matokeo ya kutakaswa ni kukamilishwa. Na aliye kamili ni Mungu. Hivyo , kukamilishwa kunahusika na mtu kushirikishwa Umungu wa pekee wa kweli.
Kunafanyikaje? 1Kor.12:13 hutuambia, “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu wayahudi au kwamba tu Wagiriki; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja”. Kumbe kubatizwa kwa roho ni kunyweshwa roho mtakatifu. Nikushirikishwa Mungu wa pekee wa kweli.
Na kwa Ubatizo huo wa kunyweshwa Roho Mtakatifu, wote watakuwa wamemvaa Kristo Yesu kuwa watoto wa Mungu wa pekee wa kweli (Gal.3:27, 26). Kwa ubatizo huo wa kunyweshwa Roho Mtakatifu, wahusika huwa ndani ya Mungu, na Mungu ndani ya nafsi husika. Nafsi husika huwa warithi wa Mungu warithio pamoja na Kristo Neno la Mungu (Rum.8:17). Watu au nafsi husika zitakuwa zimetimilika katika utimilifu wote wa Mungu (Efe.3:19; Kol.2:9-10). Kama vile mtoto wa simba alivyo simba, vivyo hivyo, mtoto wa Mungu ni Mungu (1Yoh.4:17).
KUTIMILIKA KWA SHARTI LA KUUONA NA KUUINGIA UFALME WA MUNGU
Kwa ubatizo huo wa kunyweshwa na kuvalishwa Umungu alilolitoa Bwana wetu Kristo Neno la Mungu kwamba mtu asipozaliwa mara ya pili hatauona Ufalme wa Mungu, litakuwa limetimilika (Yn.3:3; 1Pet. 1:23).
MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO (Yn.3:5)
Mtu asipozaliwa kwa maji yapi? Katika mazungumzo kati ya Kristo Yesu na Yule mwanamke Msamaria pale kisimani, Kristo Neno la Mungu alimwambia Yule mwanamke, “Kama ungalijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye nipe maji ninywe, wewe ungalimwomba Yeye Naye angalikupa maji yaliyo hai. Yeye anywae maji haya ataona kiu tena. Bali yeye anywaye maji nitakayompa mimi ataona kiu hata milele. Bali maji hayo yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji yakimbubujikia uzima wa milele” (Yn.4:10, 14).
Na katika Yn.7:37-39 Bwana Yesu Neno la Mungu anatualika, “Mtu akiona kiu na aje kwangu anywe. Aniaminiye Mimi kama vile Maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. Na Neno hilo alilisema kuhusu Roho ambaye wale waaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”.
Hivyo maji yanayohusika na ubatizo aliouleta Kristo Neno la Mungu si maji ya kumwagiwa wala kuzamishwa; bali ni maji ya kunyweshwa yakae ndani ya mtu kumbubujikia uzima wa milele, uzima ule ule wa Mungu wa pekee wa kweli.
La kukazia hapa ni kwamba Mkarismatiki kweli kweli ni Yule aliyenyweshwa Roho Mtakatifu. Na kwa tendo hilo mtu huyo yuko ndani ya Kristo Neno la Mungu na Kristo Neno la Mungu yumo ndani ya mtu ahusikaye. Hivyo mtu huwa Roho moja na Kristo Neno la Mungu. Na kwa jinsi hiyo mtu huwa mshiriki wa utimilifu wote wa Mungu. Na hapo aweza kufanya yote aliyofanya Kristo Neno la Mungu; (Yn.14:12) maana Mtendaji ni Roho Yule Yule atendaye ndani ya Kristo aliye ndani ya huyo mtu ahusikaye. Maana atendaye si huyo mtu ahusikaye, bali ni Roho Mtakatifu ambaye yuko ndani ya Kristo aliye ndani ya mtu husika. Na hivyo, kumsifu huyo mtu ni dhambi ya kumwibia Mungu Utukufu wake.
Kamusi ya Kiingereza inatuelezea msukumo wa Kikarismatiki (Charismatic Movement) kwamba ni msukumo wa kimsingi katika Makanisa ya Kikristo ambao hukazia karama au vipawa ambavyo husadikiwa kwamba vinatolewa na Roho Mtakatifu.
Mtazamo huu wa kukazia karama au vipawa hauzingatii ukweli kwamba Yule asi huwa anajiinua juu ya kila kiitwacho Mungu au cha kuabudiwa; huyu ambaye haachi kuingia katika hekalu la Mungu akijionesha nafsi yake kama kwamba yeye ndiye Mungu (2Thes.2:3-4).
Kuhusu ukweli huu, Bwana aliye Kristo Neno la Mungu anatuonya, “Na wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki; kwa maana watajitokeza makristo wa uongo, na manabii wa uongo, watatoa ishara na maajabu wapate kuwadanganya, ikiwezekana, hata hao wateule. Bali ninyi jihadharini; nimekwisha kuwaonya yote mbele” (Mk.13:21-23).
Katika hili mafundisho ya Mitume yanazidi kuweka wazi; hao waliambiwa Roho Mtakatifu atawaongoza awatie katika kweli yote:
1. “Kuja kwa Yule mwasi ni kazi ya shetani, atumiaye uwezo wote, ishara na ajabu za uongo; na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli wapate kuokolewa (2Thes.2:9-10).
2. Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni juu ya nchi mbele ya wanadamu. Naye awakosesha wale wakaao juu ya nchi, kwa ishara zile alizopewa kuzifanya mbele ya huyo mnyama (Ufu.13:13-14).
3. “Hizo ndizo roho za mashetani zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote (Ufu.16:14).
Kuhusu swala hili la ishara na ajabu, Kristo, Neno la Mungu alituonya mbele (Mk.13:23). Je, wakarismatiki tunaonyeka kiasi gani katika hili. Ikiwa watu, baada ya kupokea utakaso kwa njia ya imani katika Damu ya Yesu, hunyweshwa Roho Mtakatifu, Roho Mtakatifu huwa mkazi ndani ya watu kuwabubujikia uzima, (Yn.4:14). Huyo roho ambaye huwa anaitwa “Shuka roho, shuka na moto wako!! N.k. ni roho gani huyo kama siyo Yule aliyeshangawa na Paulo Mtume katika 2Kor.11:4? Je, huko si kumtumikia shetani badala ya Kristo Neno la Mungu?
Tukubali, tusikubali, ukweli unabaki kwamba Karismatiki Katoliki ni tunda la Vatikani II; na Mababa waliofuata waliipokea Karismatiki Katoliki kuwa ni Baraka kwa Kanisa.
Kutokana na ukweli huu, Karismatiki Katoliki inapaswa kuwa ni chombo cha utekelezaji wa fundisho la Vatikani II kama tunavyofikishiwa na Mababa Mtakatifu.
Mababa wanatutaka tuwe waaminifu kwa Injili; tuiongokee Injili kwa kina, kuwa na fikira mpya, kuwa na mtazamo mpya wa mambo, kuiheshimu kweli kuliko chochote kila; na, katika mchakato wa kutafuta kweli, namna zetu za kuelezea imani zetu kamwe zisiwe kizingiti.
Ili kuwa waaminifu kwa Injili au kuongokea Injili kwa kina kunadai utekelezaji wa sharti la kuwa mwanafunzi wa Yesu kweli kweli, nalo ni kukaa katika Neno lake (Yn.8:31-32).
Kujikita katika Uinjilishaji badala ya kujikita katika kujua kweli huishia kujawa na wafanya mazingaumbwe (Conjurers) badala ya wainjilishaji katika Karismatiki Katoliki ambao bila aibu wanajiita, “Wakarismatiki kweli kweli na wakatoliki kweli kweli. Na kwa sababu hiyo, hawatakuwa nje ya wale walioambiwa “Ninyi ni wa baba yenu ibilisi; na tamaa za baba yenu ndizo mpe ndazo kuzitenda; maana yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakusimama katika kweli. Asemapo uongo asema yaliyo yake mwenyewe; maana yeye ni mwongo na baba wa huo” (Yn.8:44).
NENO LA MUNGU NI UZIMA
1. Kumeshuhudiwa watu watatu kuondokewa na kansa ya ziwa walipojua na kuamini ukweli wa Neno la Mungu kwamba mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu na kuyachukua magonjwa yetu (Mt.8:17). Tangu tarehe 24/12/2005, mhusika mmoja wapo ni hai hadi sasa. Hata wawili waliofuata miaka ya badaye, nao ni hai.
2. Wawili kuondokewa na ukimwi wa shetani kwa kujua na kuamini kushirikishwa kwao utimilifu wote wa Mungu (1Yn.4:13; Efe.3:19; Kol.2:9-11). Badala ya ukimwi wa ibilisi wakapokea Ukimwi wa Yesu, ukamilifu au utimilifu wa kinga mwilini. Wanadunda katika uzima wa Yesu, Neno la Mungu hata sasa.
3. Kuna Mama aliyepokea kutodhurika kwa mwanawe aliyekunywa sumu ya kutibia minyanya kwa hoja kwamba Yesu Neno la Mungu amesema, “Hata mkinywa cha kufisha hakitawadhuru” (Mk.16:17-18).
Yote kwa yote, kweli, ni dawa; tena ni dawa ya uhakika; kwani kweli ni Mungu mwenyewe mwenye kuponya yote (Hek.16:12). Tena Kristo Neno la Mungu, kasha tuombea kwa Baba, “Uwatakase kwa ile Kweli; Neno lako ndiyo kweli. Nami najiweka wakfu mwenyewe ili na hao watakaswe katika Kweli” (Yn.17:17, 19). Je, inawezekana Baba kumkatalia Mwana ombi hili? Mungu hudumu wa kuaminiwa; maana hawezi kujikana mwenyewe (2Tim.2:13). Ukiwa na moyo mgumu kuupokea na kuuamini Ukweli huu ni kwa hasara yako.
Badala ya kujikita kwenye makongamano yanayogharimu muda na mali nyingi; hebu sasa Karismatiki iwe Chuo Kikuu cha Elimu ya mbinguni kwa kujikita katika Neno la Mungu (Yn.8:31-32) ili kukidhi mapenzi ya Mungu anayetaka watu wote waokolewe na kujua ile kweli (1Tim.2:4). Watu wa Mungu wanaangamia kwa kukosa maarifa (Hos.4:6). Tena watu wa Mungu wanapotea kwa kutojua Maandiko wala uwezo wa Mungu, (Mt.22:29). Karismatiki iwe chombo cha kudhihirishia njia ya wokovu.
Mungu akubariki kwa Roho wake wa Kweli wa kukuongoza akutie kwenye kweli yote (Yn.16:13) na kukuwezesha kuukulia Umungu wa pekee wa Kweli hata kumfikia Yeye katika yote (Efe.4.13-15). Yote yakiwa kwa sifa na utukufu wa Mungu wa pekee wa Kweli, kwa usalama wako na wa dunia yote Mungu aliyoiumba kwa ajili yake.
Kujigamba kwamba Umkarismatiki kweli kweli na Mkatoliki kweli bila kunyweshwa na kuvalishwa utimilifu wote wa Mungu ni kuwa mwongo na mtumishi wa Ibilisi; ni KUJILAANI.
Amini kwamba Mungu wa pekee wa kweli, Baba wa Bwana wetu Kristo Neno la Mungu, na Baba yetu, amekubariki kwa sababu ya kuikubali na kuipenda ile Kweli kwani Kweli ni Yeye mwenyewe. Kuikubali na kuipenda Kweli ndipokumkubali na kumpenda Mungu wa pekee, wa Kweli. Achana kabisa na uongo.
LUKA ROKI MAGHALI CHAMAYOMBE
0787 765 759
0714 118 428
0753 298 707
Chamayombe37@gmail.com

0 comments:

Post a Comment